Watoto hao walipigwa na radi kufuatia mvua kubwa iliyonyesha ikiambatana na upepo mkali, huku mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Hawa Jumanne akijeruhiwa kufuatia tukio hilo.
Akisimulia kwa masikitiko makubwa hali halisi ilivyokuwa, majeruhi wa tukio hilo Bi Hawa Jumanne amesema wakati mvua ikiendelea kunyesha alikuwa anakula chakula na mtoto wake ghafla alijikuta amerushwa nje na nguvu ya radi huku mwanaye akiwa anagalagala ndani ya nyumba kutokana na mshtuko wa radi hiyo.
Muuguzi Mkuu wa zamu katika hospitai teule ya rufaa Katavi, Bi Renata Kazungu ambaye amethibitisha kuwapokea watoto hao wawili wakiwa wameshapoteza maisha.
0 Comments