Meja Jenerali wa jeshi Jon Jensen wa kikosi cha walinzi hao cha Minnesota amesema wanajeshi waliosambazwa wana mafunzo ya kuwalinda raia, mali na kuhakikisha haki ya watu kuandamana kwa amani.
Hatua hiyo ilianza usiku wakati waandamanaji walipoanza kupora na kuchoma majengo kadhaa kote kwenye miji hiyo, kufuatia ghadhabu zilizochochewa na ukatili wa polisi dhidi ya Mmarekani mwenye asili ya Afrika.
Wanajeshi hao watasaidia polisi wa miji hiyo kulinda amani kuanzia leo.
0 Comments